Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea: Wabunge CCM wanajali matumbo, chama chao
Habari za Siasa

Kubenea: Wabunge CCM wanajali matumbo, chama chao

Saed Kubenea
Spread the love

SAED Kubenea, mgombea ubunge wa Jimbo la Kinondoni kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, amesema Abbas Tarimba, mgombea ubunge katika jimbo hilo kupitia CCM, ana tabia zile zile walizonazo wabunge wanaotokana na chama hicho. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Amesema, tabia ya wabunge wanaotokana na chama hicho, ni kutumikia matumbo yao na chama chao badala ya wananchi waliowaweka madarakani.

“Kila mbunge wa CCM anapokwenda bungeni, anakuwa na mambo mawili, kwanza chama chake na tumbo lake, kwa hiyo Abbas Tarimba anakwenda kutetea CCM na kutetea mchezo wake wa kamari.” amesema Kubenea

“Nimekuwa mbunge miaka mitano, nimekuwa mwandishi wa bunge kwa zaidi ya miaka 17, ninafahamu wafanyabiashara wote wa kamari na casino wanavyoteka kamati ya bajeti.”

Kubenea ambaye aliyekuwa mbunge wa Ubungo kupitia Chadema (2015 – 2020), ametoa kauli hiyo tarehe 30 Septemba 2020 katika mkutano wa kampeni uliofanyika Magomeni Mzimuni, jijini humo.

Amesema, Kinondoni inamuhitaji mtu mwenye muda wa kutosha kuwatumikia wananchi na aliyejitoa kwa dhati ambaye ni yeye.

Kubenea amesema, Tarimba ambaye ni Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti SportPesa Tanzania inayojihusisha na michezo ya bahati nasibu, hawezi kuwa na muda wa kujua shida za wa nanchi na kuzitatua.

“Wakati wa Bunge, miswada inayohusu michezo ya kamari na michezo ya bahati na nasibu, serikali inachukua mapato ya kodi nyingi, kina Abbas Tarimba wanakuja bungeni kutaka ifanyiwe marekebisho,” alisema

Kubenea alitumia fursa hiyo kuelezea mchakato wa kupata mgombea ubunge wa Kinondoni kupitia CCM jinsi chama hicho kilivyoshindwa kushughulikia malalamiko ya wale walioshiri.

“Chagueni mbunge atakayekwenda bungeni kupeleka kitu chenu, msichague mbunge ambaye hatokuwa na muda nanyi bali kwenda kutetea biashara yake na chama chake.

“Hata leo (jana) kulikuwa na msiba hapa, Tarimba ameishia pale nyumbani makaburini hakwenda, ameswalia pale, amekula pilau kisha huyo, hajapata ubunge hajakwenda kuzika, akipata ubunge je,” alihoji Kubenea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!