Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea: Tutashinda na tutatangazwa washindi
Habari za SiasaTangulizi

Kubenea: Tutashinda na tutatangazwa washindi

Spread the love

MBUNGE wa Chadema jimbo la Ubungo, Saed Kubenea amesema, ni lazima chama chake kiibuke kidedea kwenye kinyang’anyiro cha ubunge jimboni Kinondoni. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Kigogo leo Jumanne, Kubenea amesema, ushindi kwa Chadema unatokana na makosa ya mshindani wao katika kuteuwa mgombea.

“Ni lazima tutashinda uchaguzi huu. Ni kwa sababu, tuna mgombea mzuri ukilinganisha na CCM na kwamba chama hicho tawala kimedharau wananchi,” ameeleza Kubenea.

Amesema, “kuna wanaopita mitaani na kusema, hata tukishinda hatutangazwa. Nataka kuwaambia, hawatujui. Nataka kuwaambia tutashinda na tutangazwa.”

Uchaguzi mdogo wa ubunge katika jimbo la Kinondoni unafanyika kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa mbunge wake, Maulid Said Mtulia, aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kupitia Chama cha Wananchi (CUF).

Kubenea ndiye meneja kampeni wa mgombea ubunge wa Chadema katika jimbo la Kinondoni, Salum Mwalimu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!