SAED Kubenea, mgombea ubunge katika Jimbo la Kinondoni kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, amesema hakugombea ubunge katika Jimbo la Ubungo ili kutogawa kura za upinzani. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea).
Akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni za mgombea udiwani kwenye Kata ya Tandale, jimboni humo Mohammed Ismail, tarehe 13 Septemba 2020 amesema, hayupo radhi kugawa kura za upinzani.
”Nimefikia uamuzi wa kuacha kugombea Ubungo kwasababu ningeng’ang’ania kugombea, ningegawa kura na hatimaye CCM ishinde, sitaki kushiriki dhambi hiyo,” amesema Kubenea na kuongeza:
“Nimegombea Kinondoni kwa kuwa, naijua vizuri na nimeshiriki shughuli nyingi nikiwa kwenye Manspaa ya Kinondoni kwa mwaka mmoja na nusu.”
Amesema, ataendelea kutetea ajenda za wananchi na kwamba atahakikisha anamaliza athari za mafuriko katika jimbo hilo.
“Разум, однажды расширивший собственные границы, никогда не воротится в бывшие.” – доказывал А. Эйнштейн. Превеликое спасибо только за то, что Вы, своими заметками, позволяете разуму перейти за пределы привычных границ.