Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea kutoa mil 14 kujenga daraja Mabibo
Habari za Siasa

Kubenea kutoa mil 14 kujenga daraja Mabibo

Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo, akizungumza na wapiga kura wake
Spread the love

MBUNGE wa Ubungo, Saed Kubenea ameahidi kutoa Sh. 14 milioni kwa ajili ya kujenga kivuko kilichoosombwa na mafuriko kilichopo Mabibo Sahara. Anaripoti Hamisi Mguta … (endelea). 

Kubenea ametoa ahadi hiyo leo alipotembelea eneo hilo kusikiliza kero za wakati hao wa Mabibo Sahara zikiwemo na kivuko hicho cha waenda kwa miguu ambacho kilisombwa na mafuriko kutokana na mvua kubwa zilizonyesha hivi karibuni.

Wakati wa maeneo hayo wamekuwa na kero ya kuvuka katika eneo hilo baada ya madaraja mawili kusombwa na maji, kabla ya kikundi cha vijana kujenga daraja la magogo ambalo wananchi wanalipia sh 200 ili kupita.

Mbali na ahadi hiyo, mbunge alitoa kiasi cha sh 150,000 ili vijana hao wawaruhusu wananchi kupita bure kabla ya kujenga kivuko hicho kwa kiwango kama ilivyokuwa hapo awali.

Hata hivyo mbele ya mbunge kuliibuka mabishano kati ya wananchi kwa kila mmoja akitaka daraja lijengwe eneo ambalo yeye anaona sahihi. Mgogoro huo ulimalizwa na Kubenea kwa kuwaahidi wataalamu kutoka manispaa watafika kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu ili kujua eneo sahihi la daraja linatakiwa kujengwa wapi.

Fatma Said mwananchi wa eneo hilo ambaye alimwelezea mbunge umuhimu wa kuhamisha daraja hilo kwenda katika eneo lingine lisilo na makazi ya watu.

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!