Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea kumaliza tatizo la takataka Kinondoni
Habari za Siasa

Kubenea kumaliza tatizo la takataka Kinondoni

Spread the love

SAED Kubenea, mgombea ubunge Kinondoni kupitia Act-Wazalendo ameahidi kumaliza changomoto ya uchafuzi wa mazingira kwa kuanzisha kiwanda kitachochakata takataka kuwa mbolea. Anaripori Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Kubenea alitoa ahadi hiyo jana Jumatano tarehe 17 Septemba 2020 alipokuwa akimnadi mgombea udiwani wa Tandale, Mohammed Kassim katika Uwanja wa Fisi.

Alisema Kinondoni haitakuwa na msongamano wa takataka na kwamba hizo zitageuka kuwa fursa.

“Takataka zitakuwa fursa, itakuwa mtu anaziuza kwenye viwanda na baadaye zitabadilishwa kuwa mbolea. Kinondoni haitakuwa na takataka,” alisema.

Kubenea alisema, anaijua Kinondoni na kwamba amekuwa kwenye baraza la madiwani wa manspaa ya Kinondoni kwa mwaka mmoja na nusu akiwa Mbunge wa Ubungo kupitia Chadema kati ya mwaka 2015-2020.

Alisema kuwa akiwa kwenye Manspaa hiyo alipigania wananchi wa Kinondoni wasibomolewe makazi yao ndio sababu zoezi hilo lilisitishwa.

Kubenea alisisitiza dhamira yake ya kumaliza athari za mafuriko kwenye jimbo hilo kwa kuwashawishi wadau wa maendeleo kuendelea na mradi kupanua mto msimbazi na mto ng’ombe sambamba na kuweka bustani ya utalii.

Naye Kassim akijinadi kwa wananchi, alisema akifanikiwa kuwa diwani ataupaisha mchezo wa ndondi (boxing).

Kassim alisema eneo la Tandale lina vipaji vingi vya mchezo wa ngumi hivyo atawatengenezea mazingira mazuri ya mchezo huo.

“Najua hapa Tandale kuna vipaji vingi vya mchezo wa ngumi, hata mimi mwenyewe ni mwanamichezo, nitahakikisha wanamichezo wanafahamika nje na ndani ya nchi,” amesema Kassim huku akishangiliwa na wananchi waliojitikeza kwenye mkutano huo.

Kassim alisema akichaguliwa yeye katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika tarehe 28 Oktoba 2020 atahakikisha Tandale ina maendeleo ya kiuchumi, michezo na miundombinu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!