Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea, Komu waanza kuhojiwa na Kamati Kuu Chadema
Habari za SiasaTangulizi

Kubenea, Komu waanza kuhojiwa na Kamati Kuu Chadema

Anthony Komu Mbunge wa Moshi Vijijini na Saed Kubenea wa Ubungo
Spread the love

WABUNGE Saed  Kubenea (Ubungo) na Anthony Komu (Moshi Vijijini) wameanza kuhojiwa na Kamati Kuu ya Chadema katika kikao cha kamati hiyo kinachoendelea leo Jumatano Oktoba 17, 2018 katika ukumbi wa Ledger Plaza katika Hoteli ya Bahari Beach. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kikao hicho pamoja na ajenda nyingine lakini pia kimekutana kuwajadili wabunge hao wawili baada ya kudaiwa kupanga mpango hasi dhidi ya Meya wa Ubungo, Boniface Jacob kupitia kile kinachodaiwa sauti iliyotengeneza ya mpango huo.

Kubenea na Komu katika siku za hivi karibuni wamezua mjadala ndani na nje ya chama hicho baada ya kuvuja kwa sauti hiyo ambayo inadaiwa ni mazungumzo kati ya wabunge hao.

Wabunge hao waliwasili ukumbi hao majira ya saa 8:01 mchana ambapo baada ya kupewa maelezo, Komu ndiyo alikuwa wa kwanza kuingia kuhojiwa mbele ya kamati hiyo huku Kubenea akisubiri muda wake kuitwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!