Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea aunga na familia kumsaka mwanafunzi aliyesombwa na maji
Habari za Siasa

Kubenea aunga na familia kumsaka mwanafunzi aliyesombwa na maji

Spread the love

MBUNGE wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), katika jimbo la Ubungo, leo Jumapili, tarehe 20 Oktoba, aliungana na mamia ya wananchi katika kutafuta mwili wa mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Shule ya Sekondari Makoka, Rashid Charu Makoye. Anaripoti Hamis Mguta…(endelea).

Mwanafunzi huyo alitoweka tangu siku ya Alhamisi baada ya kusombwa na maji wakati alipokuwa akivuka mto Gide, mpkani mwa mtaa wa Kimara Bauti, kata ya Kimara na Makoka, mtaa wa Makuburi.

Tukio hilo lilitokea majira ya saa mbili asubuhi, wakati mwanafunzi huyo alipokuwa akielekea shuleni kwa ajili ya masomo yake.

Akiwa na baadhi ya maofisa wa Polisi waliokuwa wameongoza na mbwa maalum wa kutafuta miili ya watu waliopatwa na maafa kama kusombwa na maji na kufukiwa na kifusi, Kubenea alitumia nafasi hiyo kuwapa pole ndugu wa kijana huyo na kuwaeleza kuwa yuko pamoja nao katika kipindi hiki kigumu wanachopitia.

https://youtu.be/v_NU-uWRRXY

Kwa mujibu wa familia yake, Rashidi ni mkazi wa Mbezi Makabe na kwamba tokea siku alipotumbukia kwenye mto huo kumekuwa na jitihada za kumtafuta, zikiongozwa na mwenyekiti wa Mtaa wa Makoka, Emmanuel Benjamin Akyoo na mbunge huyo.

Kubenea alifika eneo hilo majira ya saa nane mchana na kulakiwa na mamia ya wananchi waliokuwa wamejiukusanya kupokea taarifa za kutokea kwa ajali hiyo na hatua zilizochukuliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!