Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kuanguka Trump, mwanasheria mkuu ang’oka
Kimataifa

Kuanguka Trump, mwanasheria mkuu ang’oka

Spread the love
MWANASHERIA Mkuu wa Marekani, Jeff Sessions amejiuzulu wadhifa huo akitekeleza agizo la Rais Donald Trump, lililomtaka kuachia ngazi. Yanaripoti Mashirika ya Kimataifa …(endelea).
Trump alitoa agizo hilo jana tarehe 7 Novemba 2018, ikiwa ni masaa 24 baada ya chama chake cha Republican kupoteza udhibiti wake katika Bunge la Wawakilishi, kufuatia kuanguka katika uchaguzi wa kati kati ya muhula uliofanyika juzi Jumanne.
Katika barua yake ya kujiuzulu aliyoiwasilisha hapo jana, Sessions aliandika kwamba uamuzi wake wa kujiuzulu unatokana na agizo la Trump, lililomtaka kujiuzulu.
Kupitia akaunti yake ya Twitter, Trump alimpongeza Sessions kwa hatua yake ya kujiuzulu na utumishi wake wakati akiwa Mwanasheria Mkuu.
Katika hatua nyingine, Trump amemteua Matthew Whitaker kukaimu nafasi ya Mwanasheria Mkuu hadi pale atakapoteuliwa mtu kushikiliwa wadhifa huo.
Awali Trump alikuwa amekosana na Whitaker kutokana na kutofurahishwa kwake na hatua ya kujiondoa katika uchunguzi wa FBI kuhusu madai ya Urusi kuingilia uchaguzi wa Marekani 2016. Alidai kuwa Sessions alikuwa na msimamo dhaifu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!