Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Korea washangilia bomu la Nyuklia
Kimataifa

Korea washangilia bomu la Nyuklia

Moja ya kombora la Korea Kaskazini baada ya kurushwa
Spread the love

KOREA Kaskazini imefanya sherehe kubwa kwa ajili ya kuwaenzi wanasayansi waliofanikisha majaribio makubwa ya bomu la Nyuklia nchini humo, anaandika Irene Emmanuel.

Sherehe hiyo imefanyika katika Mji Mmkuu, Pyongyang huku wananchi wakishangilia wanasayansi waliokuwa ndani ya basi katika barabara kuu za mji huo.

Wananchi walijumuika katika Uwanja wa Kim II-Sung yu kuwapongeza wanasayansi hao.
Siku ya Jumapili Korea Kaskazini ilifanyia jaribio kwa mafanikio bomu la Nyuklia aina ya Hydrogen lenye uwezo wa kufanya uharibifu.

Hili ni jaribio la sita kuhusu majaribio ya Nyuklia nchini humona kwamba lilisababisha mtetemeko wa ardhi wenye ukubwa wa 6.3 kwa kipimo cha rishta.

Korea Kaskazini imefanya jaribio hilo licha ya taharuki kutanda katika Peninsula ya Korea na vikwazo vya kila mara kutoka Marekani na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa dhidi yake.

Serikali ya Korea Kaskazini inasisitiza kuwa inalazimika kumiliki silaha za Nyuklia kwa lengo la kujihami kutokana na vitisho vya Marekani vya kuivamia kijeshi kwa mabomu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!