Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Korea Kaskazini yazidi kuililia Marekani
Kimataifa

Korea Kaskazini yazidi kuililia Marekani

Rais wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un
Spread the love

SERIKALI ya Korea Kaskazini imeionya Marekani isitumie njia za vikwazo zaidi wala za kijeshi dhidi ya Pyongyang, anaandika Hellen Sisya.

Wizara ya Mambo ya Nje ya Korea Kaskazini imetoa taarifa ya kuionya Washington, kwamba iwapo itatumia vikwazo zaidi dhidi yake au njia ya kijeshi, basi itakabiliwa na jibu kali zaidi.

Taarifa iliyotolewa na wizara hiyo imesema kuwa, majaribio ya kombora la balestiki yaliyofanywa hivi karibuni na Pyongyang ni onyo kwa Marekani.

Ijumaa iliyopita, Korea Kaskazini ililifanyia majaribio kombora lake la balestiki la kuvuka mabara kwenda katika maji ya Japan.

Baada ya jaribio hilo, Kim Jong-un, kiongozi wa nchi hiyo alitangaza kuwa jaribio hilo limethibitisha kwamba, sasa ardhi yote ya Marekani inaweza kulengwa kwa makombora ya Pyongyang.

Kwa mara kadhaa Korea Kaskazini imekuwa ikisisitiza azma yake ya kuendelea kujiimarisha kijeshi kwa silaha za nyuklia hadi pale Marekani na washirika wake watakapositisha vitisho dhidi yake.

Wakati huo huo, habari zinaarifu kwamba raia wa Korea Kaskazini wamepatwa na furaha baada ya serikali kufanya jaribio la kombora jipya siku ya Ijumaa iliyopita. Televisheni ya APTN imetangaza kuwa, baada ya jaribio hilo wakazi wa miji kadhaa walikusanyika katika viwanja mbalimbali na kushangilia hatua hiyo ambayo wameitaja kuwa ni ushindi mkubwa dhidi ya Marekani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!