Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Korea Kaskazini yazidi kuichokonoa Japan
Kimataifa

Korea Kaskazini yazidi kuichokonoa Japan

Moja ya kombora la Korea Kaskazini baada ya kurushwa
Spread the love

KOREA Kaskazini imeendelea kuichokonoa Japan kwa kurusha kombora lingine la masafa marefu ambalo linasadikika limedondokea katika bahari ya Japan, anaandika Catherine Kayombo.

Kombora hilo lililorushwa kutoka Bangyon Kaskazini mwa mkoa wa Pyongan lilisafiri umbali wa kilomita 930 kwa dakika 40, siku ya Jumanne.

Tokyo imesema kuwa kombora hilo huenda lilianguka katika eneo la kiuchumi la bahari ya Japan, lakini hawakueleza madhara yaliyosababishwa na kombora hilo.

Korea Kaskazini imeongeza viwango vya majaribio vya makombora yake katika miezi ya hivi karibuni, hili likiwa kombora la 11 mwaka huu, kufuatiwa jaribio lake la mwisho mwezi Mei ilirusha makombora yake katika nyakati tofauti yote yakielekezewa bahari ya Japan.

Kombora hilo limerushwa ikiwa ni siku moja baada ya Rais wa Marekani, Donald Trump kuzungumza kwa simu na Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe na Rais wa China, Xi Jinping kuhusu Korea Kaskazini.

Viongozi hao walithibitisha jitihada zao za kuhakikisha kuwa hakuna utumizi wa nyuklia katika nchi ya Korea Kaskazini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!