Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Koffi Olomide akumbwa na jinai ya ubakaji
Michezo

Koffi Olomide akumbwa na jinai ya ubakaji

Spread the love

NYOTA wa muziki wa Rhumba nchini Kongo, Antonie Agbepa Mumba maarufu kwa jina la Koffi Olomide amehukumiwa kifungo cha miaka miwili jela au kulipa faini katika Mahakama ya Nanterre nchini Ufaransa baada ya kukutwa na hatia ya kumbaka mnenguaji wake wakati akiwa na umri wa miaka 15. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Hukumu hiyo iliyotolewa jana tarehe 18 Machi 2019 na Mahakama ya Nanterre ambapo pia ilimtaka Olomide (62) kulipa faini yenye kiwango sawa na gharama za kuwasaidia wanawake watatu wengine walioingia nchini Ufaransa kwa njia haramu.

Pia, ilimtaka kumlipa mnenguaji huyo Euro 5,000 kama fidia ya madhara aliyomsababishia alipomfanyia ukatili huo.

Mnamo mwaka 2012 Olomide alifunguliwa mashtaka ya ubakaji na wanenguaje wake wanne, wakimtuhumu mbele ya mahakama kwamba aliwanyanyasa kingono katika nyakati tofauti mwaka 2002 na mwaka 2006 nchini Kongo na Ufaransa.

Katika malalamiko yao, wanenguaji hao waliiambia mahakama hiyo kuwa Olomide aliwazuia kwa lazima nyumbani kwake iliyoko nje ya mji wa Paris nchini Ufaransa,  na kwamba walifanikiwa kutoroka licha ya kwamba walishindwa kurudi Kongo kutokana na kuogopa kutafutwa na kulipizwa kisasi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!