Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Michezo Kocha Simba: Yanga walikuwa wanazuia
Michezo

Kocha Simba: Yanga walikuwa wanazuia

Spread the love

KOCHA wa Simba, Sven Vandebroeck amesema “kuLikuwa  na timu moja inacheza mpira na nyingine inazuia, nawapongeza wachezaji wangu kwa kucheza vizuri na ninafuraha kwa kile walichokionesha.” Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Sven amesema hayo mara baada ya kumalizika kwa mchezo kati ya Yanga dhidi ya Simba uliochezwa kwenye Uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam.

Aidha kocha huyo ameendelea kusema kuwa kipindi cha kwanza hakikuwa kizuri kwa upande wao kwa sababu kasi ya mchezo ilikuwa chini lakini pia mwamuzi alisababisha kutokea kwa jambo hilo

“Kipindi cha kwanza hatukuwa na hali nzuri na mwamuzi alikuwa anatuzuia mara kwa mara lakini kipindi cha pili tulimiliki kiufundi na nguvu” aliongezea kocha huyo.

Bao la kusawazisha la Simba lilifungwa dakika ta 86 na beki wake raia wa Kenya Josh Onyango kwa mpira wa kona mara baada ya Yanga kutangulia katika dakika 31′ kwa bao lilifungwa na Michael Sarpong kwa njia ya penati.

Kwa matokeo haya Simba itaendelea kubakia nafasi ya tatu ikiwa na alama 20 nyuma ya Yanga yenye pointi 24 kwenye nafasi ya pili.

1 Comment

  • Kadi ya mkude kama hakutkana refa Na kuangushwa kwa Luis ilikua Ni njama ya kuichngnya Simba kmchezo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Ujanja ni kubeti na Meridianbet

Spread the love  JUMAPILI ya leo imekaa kihela hela sana ndani ya...

Michezo

Anza Jumamosi yako na mkwanja wa Meridianbet

Spread the loveJumamosi ya leo ODDS zimekaa kijanja sana ndani ya Meridianbet...

error: Content is protected !!