Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Kocha mpya Simba: Namjua Kagere
Michezo

Kocha mpya Simba: Namjua Kagere

Spread the love

 

KOCHA mpya wa timu ya Simba, Didier Gomes amesema kuwa ameifuatilia kwa karibu Ligi Kuu ya Tanzania Bara na kuwafahamu baadhi ya wachezaji ikiwemo Meddie Kagere ambaye alimfundisha alipokuwa kwenye klabu ya Rayol Sport ya nchini Rwanda. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Kocha huyo ametua nchini jana na kujiunga na klabu ya Simba kwa mkataba wa miaka miwili leo Jumapili 24 Januari 2021.

Wakati akijibu swali la mwandishi wa habari kwa namna gani ameifuatilia Ligi Kuu ya Tanzania na kujibu kuwa ameifuatilia Ligi hii kwa muda mrefu kwa kuwa inaendelea kukua taratibu kwa siku za hivi karibuni.

“Naijua na nimeifuatilia Ligi ya Tanzania kwa kuwa ni moja ya Ligi nzuri na inakuwa kila siku na hata hivyo nawajua baadhi ya wachezaji akiwemo Meddie Kagere ambaye nilimfundisha nikiwa nchini Rwanda nikiwa na klabu ya Rayon Sports,” alisema kocha huyo.

Kagere ambaye alikuwa hapati nafasi ya kuanza kwenye kikosi cha kwanza cha kocha aliyeondoka kutokana na mfumo wake wa kutumia mshambuliaji mmoja na kuamua kumtumia zaidi John Bocco.

Pengine ujio wa Gomes huenda ukampa tena nafasi mchezaji huyo ambaye alikuwa mfungaji bora wa klabu hiyo pamoja na Ligi Kuu kwenye msimu uliomalizika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!