MSHAMBULIAJI Dickson Ambundo wa klabu ya Alliance Accademy na Kocha Mkuu wa KMC, Etiene Ndayiragije wameibuka vinara kwenye tuzo za mwezi Januari zinazotolewa na Bodi ya Ligi baada ya kufanya vizuri kwenye michezo yao. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea)
Ambundo ameibuka kinara kwenye tuzo hiyo baada ya kuwashinda mlinda mlango wa KMC, Juma Kaseja na mshambuliaji wa Coastal Union, Ayoub Lyanga huku kocha Etiene alifanikiwa kuwapiku makocha Malale Hamsini ambaye anakinoa kikosi cha Alliance na Amri Said wa Biashara United.
Ndayiragije amefanikiwa kuiongoza KMC katika michezo 24 ya Ligi Kuu Tanzania Bara toka ilipopanda daraja na kufanikiwa kujikusanyia alama 35 na kushika nafasi ya tano kwenye msimamo.
Washindi wa tuzo hiyo katika msimu huu wa 2018/19 watajinyakulia kitita cha Sh. 1 milioni kutoka kwa mdhamini mkuu Biko Tanzania.
Leave a comment