Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Michezo Klopp awagwaya Leicester City
Michezo

Klopp awagwaya Leicester City

Spread the love

MENEJA wa klabu ya Liverpool, Jurgen Klopp ameonekana kuwahofia dhidi klabu ya Leicester City katika kuelekea kwenye mchezo wao wa ligi kuu nchini Uingereza utakaopigwa siku ya Jumamosi kwenye dimba la King Power. Anaripoti Kelvin Mwaipungu …. (endelea).

Klopp ambaye amechaguliwa kuwania tuzo ya kocha bora wa mwezi wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema kwa sasa Leicester wanaonekana kubadili aina yao ya mchezo, wanacheza vizuri na kwa kujiamini.

“Unaweza kuona kocha Claude Puel anafanya kazi nzuri, amebadilisha jinsi ya kucheza, ni mpira mzuri wanaocheza na kujiamini zaidi. Utakuwa mchezo mgumu kwetu,” amesema Klopp.

Liverpool ambayo mpaka sasa imeshinda michezo yao miwili iliyopita inapewa nafasi kubwa ya kutwaa taji la Ligi Kuu nchini humo kutokana kuwa na kikosi kizuri na kilichofanya vizuri katika msimu uliomalizika wa michuano ya klabu bingwa barani Ulaya licha ya kupoteza mchezo wao wa fainali dhidi ya Real Madrid.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Ujanja ni kubeti na Meridianbet

Spread the love  JUMAPILI ya leo imekaa kihela hela sana ndani ya...

Michezo

Anza Jumamosi yako na mkwanja wa Meridianbet

Spread the loveJumamosi ya leo ODDS zimekaa kijanja sana ndani ya Meridianbet...

error: Content is protected !!