MBUNGE wa Viti Maalum (CUF), Rukia Ahmed ameitaka serikali kuwaondolewa ukali wa gharama za matibabu, waathirika wa magonjwa yasiyo ya kuambukiza hasa kisukari na saratani. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).
Rukia ametoa wito huo wakati akiuliza swali kwa Wizara ya Afya, akisema kuwa magonjwa yasiyo ya kuambukiza, ikiwemo kisukari na saratani matibabu yake yamekuwa ghali na hayako ya moja kwa moja, na kuitaka serikali kutoa msimamo wake katika kuboresha huduma ya waathirika wa magonjwa haya hususan kwenye matibabu.
Akijibu swali hilo kwa niaba ya Waziri wa Afya, Waziri wa Maliasili na Utalii, Hamis Kigwangalla amesema serikali inaendelea kuhimiza wananchi hasa waathirika wa magonjwa yasiyo ya kuambukiza kujiunga na bima ya afya ili kupunguza mzigo wa gharama za matibabu.
“Gharama za magonjwa yasiyo ya kuambikiza ni kubwa mno, serikali imeanzisha mkakati wa kuhamasisha watu kuishi maisha ya afya, kuangalia vyakula wanavyokula, kufanya mazoezi, hivyo ili kuepuka gharama za kutibu . Tunaendelea kuhamasisha zaidi kinga kuliko tiba, kuna mkakati watu wote wawe na bima ya afya ili huo mzigo wa gharama usiweze kuwa mkubwa na badala yake ubebwe na jamii,” amesema.
Leave a comment