Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Kipigo cha bao 2 – 0, chaifanya Stars kuweka rekodi CHAN
Michezo

Kipigo cha bao 2 – 0, chaifanya Stars kuweka rekodi CHAN

Spread the love

BAADA ya kukubali kipigo cha mabao 2 – 0, dhidi ya Zambia kwenye michuano ya kombe la Mataifa Afrika, Timu ya Taifa ya Tanzania imeweka rekodi ya kuwa timu ya kwanza kufungwa mabao mawili toka kuanza kwa michuano hiyo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea). 

Michuano hiyo ambayo ilianza siku ya Jumamosi tarehe 16 Januari 2021 mpaka sasa imepigwa jumla ya michezo saba, huku kukiwa hakuna timu iliyopoteza kwa mabao mawili.

Siku ya ufunguzi ilipigwa michezo miwili ambapo wenyeji Cameroon waliibuka na ushindi wa bao 1-0, mbele ya Zimbabwe, huku mchezo wa pili uliwakutanisha Mali ambao waliibuka na ushindi wa bao1-0, dhidi ya Burkina Faso.

Michezo mingine iliwakutanisha Libya ambao walikwenda sare ya bila kufungana dhidi ya Niger, huku Morocco wakifanikiwa kuwalaza Togo kwa bao 1-0.

Congo walikubali kichapo cha bao 1-0, kutoka kwa ndugu zao Congo Dr, na mchezo mwengine uliwakutanisha Rwanda dhidi ya Uganda ambao walitoka suluhu ya bila kufungana.

Stars ambayo ilicheza mchezo wake wa kwanza wa kundi D na kupoteza pointi tatu ambazo zingeweza kuwaweka vizuri kwenye msimamo.

Mabao ya Zambia kwenye mchezo huo yalifungwa na Colkins Sikombe kwa njia ya mkwaju wa penalti mara baada ya mlinzi wa Taifa Stars, Shomary Kapombe kunawa mpira kwenye eneo la hatari.

Bao la pili la Zambia likapachikwa wavuni na Emmanuel Chabula na kukamilisha idadi ya mabao hayo kwenye mchezo huo.

Kwa mantiki hiyo Stars imebakiksha michezo miwili dhidi ya Guimea na Mali ili kujua hatma yao kufuzu katika raundi inayofuata.

Michuano hiyo inafanyika nchini Cameroon na ilifunguliwa na Rais wa Shirikisho la Mpira Duniani (FIFA), Gianni Infantino ambaye alishuhudia mchezo wa ufunguzi kati ya wenyeji Cameroon dhidi ya Zimbabwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

error: Content is protected !!