Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kiongozi wa waasi, wenzake 18 wahukumiwa kifo
Habari Mchanganyiko

Kiongozi wa waasi, wenzake 18 wahukumiwa kifo

souleymane keita, Kiongozi wa waasi wa kundi la Ansar Dine la Iyad Ag Ghali
Spread the love

SOULEYMAN Keita, kiongozi wa kundi la waasi la Ansar Dine la Iyad Ag Ghali nchini Mali na wenzake 18, mwishoni mwa wiki wamehukumiwa  kifo baada ya kukutwa na hatia ya ugaidi. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa ……..(endelea).

Mahakama nchini Mali, imewahukumu kifo kwa kukutwa na hatia ya ugaidi ikiwa ni pamoja na kumiliki silaha za kivita pia kushiriki mauaji ya raia wasio na hatia.

Keita na wenzake, wametajwa kushirkiki kwenye shambulio lililotokea katika Mji wa Konna mwaka 2013 na kusababisha mauaji ya watu wengi.

Mahakama nchi ni humo imeeleza, watu hao wanaojiita wana jihadi wanaojinasibisha na Uislam, wamekuwa wakishiriki mashambulizi kadhaa kwenye mji huo ulio Kusini mwa Mali pamoja na nchi za Cameroon na Burkina Faso.

Waasi

Baada ya shambulizi lililotekelezwa na akina Keita, vikundi vya usalama vya Ufaransa vilivyokuwepo Mali, vililazimika kuingilia kati na kuwatimua wapiganaji hao.

Keita anatajwa kuwa kiongozi hatari anayeendesha operesheni ya kusaka wapiganaji wapya wa kundi la Ansar Dine, na mara kwa mara amekuwa akishiriki mashambulio kwenye mipata ya nchi mbili zinazopakana na Mali.

Keita alikamatwa mwaka 2016 akiwa na wenzake wawili kutoka Burkina Faso, baada ya kufikishwa mahakamani na wenzake, walikiri kufanya mashambulio katika maeneo mbalimbali katika nchi hizo tatu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!