Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kilimanjaro: Majimbo 9, watia nia 124 CCM
Habari za Siasa

Kilimanjaro: Majimbo 9, watia nia 124 CCM

Spread the love

IDADI ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika majimbo tisa mkoani Kilimanjaro, wanaotaka kuwa wabunge mpaka sasa imefika 124. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro … (endelea).

Kwa mujibu wa Jonathan Mabihya, Katibu wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro ni kwamba, mpaka tarehe 6 Julai 2020, wanachama hao walikuwa tayari wamejitokeza kuonesha nia hiyo.

“Mpaka tarehe 6 Julai mwaka huu, tumepokea jumla ya wanachama 124. Ni wanachama ambao wanaoonesha nia ya kuomba kuteuliwa kugombea ubunge katika majimbo tisa ya mkoa huu,” amesema.

Majimbo tisa ya mkoa huo na idadi ya watia nia waliojitokeza kwenye mabano ni Rombo (14), Same Magharibi (13), Hai (8), Moshi Mjini (8), Moshi Vijijini (22), Same Mashariki (16), Siha (7), Mwanga (23) na Vunjo (13).

Mabihya amesema, matakwa ya Katiba ya chama hicho ni kuwa, wakurugenzi wa uchaguzi ni makatibu wa chama wa ngazi husika.

CCM imeeleza, wanachama walio na nia ya kuwania udiwani, uwakilishi na ubunge, wataanza kuchukua tarehe 14 – 17 Julai 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!