Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kikwete, Cheyo kuwamwakilisha Rais Magufuli kuapishwa Mnangagwa
Habari za Siasa

Kikwete, Cheyo kuwamwakilisha Rais Magufuli kuapishwa Mnangagwa

Spread the love

DK. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, anatarajiwa kumwakilisha Rais John Magufuli katika sherehe za kuapishwa wa Emmerson Mnangagwa, Rais Mteule wa Jamhuri ya Zimbabwe zitakazofanyika Jumapili tarehe 26 Agosti, 2018 katika uwanja wa michezo wa Taifa Mjini Harare. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa kwa vyombo vya habari leo tarehe 25 Agosti, 2018 na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu.

Taarifa hiyo ya Ikulu imeeleza kuwa, Rais Magufuli amemtuma Dk. Kikwete kumwakilisha ambapo atafuatana na Phillip Mangula, Makamu Mwenyekiti wa CCM na John Cheyo, Mwenyekiti wa chama cha UDP.

Rais Mnangagwa ataapishwa kesho kuongoza Zimbabwe baada ya kushinda katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 30 Julai, 2018 ikiwa anapokea kijiti kutoka kwa Robert Mugabe aliyekuwa Rais wa nchi hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!