Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kigogo wa Acacia kizimbani kwa utakatishaji fedha
Habari Mchanganyiko

Kigogo wa Acacia kizimbani kwa utakatishaji fedha

Spread the love

ASA Mwaipopo (55), Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni za Madini za Bulyanhulu, North Mara na Pangea zilizokuwa chini ya Acacia, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa mashtaka tisa yanayomkabili ikiwemo utakatishaji fedha na kughushi, na kujipatia dola za marekani 840,000. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Mwaipopo amesomewa mashtaka hayo leo tarehe 23 Oktoba 2018 na Mawakili wa Serikali, Faraja Nchimbi na Jacqline Nyantori mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi.

Upande wa mashtaka umedai kuwa, Mwaipopo ametenda makosa hayo ya kula njama, kuongoza uhalifu wa kupangwa, kughushi, ukwepaji kodi na utakatishaji fedha, katika kipindi cha Aprili 11 mwaka 2018 na Juni 30 mwaka 2017.

Hata hivyo, kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 31 Oktoba 2018 kutokana na upande wa mashtaka kutokamilisha upelelezi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

error: Content is protected !!