Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Kifafa ugonjwa unaotaabisha wakazi Wilaya ya Ulanga
Afya

Kifafa ugonjwa unaotaabisha wakazi Wilaya ya Ulanga

Dk. Faustin Ndungulile
Spread the love

GODLUCK Mlinga, Mbunge wa Ulanga (CCM) amesema kuwa, Wilaya ya Ulanga inaongoza kwa kuwa na wagonjwa wa kifafa Tanzania na duniani. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Mlinga ametoa kauli hiyo leo bungeni wakati akiuliza swali la nyongeza. Alitaka kujua, ni lini serikali itaweza kutoa dawa za kutosha kwa wagonjwa wa kifafa katika wilaya hiyo iliyopo kwenye Mkoa wa Morogoro?

“Kwa kuwa Wilaya ya Ulanga ni kinara wa ugonjwa wa kifafa duniani, na kwa kuwa kifafa kinaendana na ugonjwa wa akili, na wagonjwa wa kifafa wanaweza kuanguka muda wowote katika maji au kwenye moto. Je, ni lini serikali itaweza kutoa dawa za kutosha kwa watu wenye ugonjwa huo,” amehoji Mlinga.

Awali katika swali la msingi Edward Mwalongo, Mbunge wa Njombe Mjini (CCM) alitaka kujua, serikali inawahudumiaje wagonjwa wa akili wanaozurura mitaani hasa katika masuala ya matibabu, mavazi na makazi.

Akijibu maswali hayo Dk. Faustine Ndugulile, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto amekiri kwamba, Ulanga kuna tatizo la kifafa pia kiasi cha dawa zinapelekwa eneo hilo.

Kuhusiana na wagonjwa wanaorandaranda, Dk. Ngugulile amesema, kwa mujibu wa sheria ya afya ya akili ya mwaka 2008, inawataka ndugu na jamii kuibua wagonjwa wa akili na kuwapeleka kwenye vituo vya kutolea huduma.

“Wagonjwa wakishapata nafuu, huruhusiwa kwenda kukaa na familia zao na kwenye jamii wanazotoka. Jukumu la kwanza la kulinda afya huanzia katika ngazi ya familia lakini jamii zetu zimekuwa zikiwanyanyapaa, kuwabagua na kuwatenga wagonjwa wa akili,”amesema.

Amesema, kwa mujibu wa sheria ya afya ya akili ya mwaka 2008, sehemu ya tatu kifungu cha sheria namba 9 kifungu kidogo 1-3 imeeleza wazi kuwa, ofisa wa polisi, ofisa usalama na ofisa ustawi wa jamii ngazi ya wilaya, wana jukumu la kubainisha mtu yeyote anayerandaranda kwa kutishia amani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!