Tuesday , 19 March 2024
Habari za Siasa

Kibatala amnasua Sugu

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi-Mbeya imewaachia kwa dhamana washtakiwa Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga katika kesi. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Watuhumiwa hao wanashtakiwa kwa kosa kutumia lugha ya fedheha kwa Rais John Magufuli ambapo walinyimwa dhamana kutokana upande wa jamhuri kupinga dhamana yao mahakamani hapo.

Leo wakili wa utetezi Peter Kibatala aliieleza mahakama kuwa upande wa Jamhuri hauna hoja za kuendelea kushikilia dhamana ya watuhumia kutokana na kufunga pazia la ushahidi mahakamani.

Upande wa Jamhuri umewasilisha mashahidi sita mahakamani hapo.

Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Michael Mteite, amewapa dhamana watuhumiwa hao.

Watuhumiwa hao walijidhamini wenyewe kwa kusaini hati ya Sh. Milioni tano kila mmoja.

Mawakili wa pande zote mbili walikubaliana kuwasilisha majumuisho ya shauri hilo tarehe 19 Februari.

Kesi hiyo itatajwa tena Februari 26 mwaka huu ambapo mahakama hiyo itatoa hukumu ya kwamba Sugu na mwenzie wana hatia au laa.

Kama mahakama itawakuta na hatia watuhumiwa hao wanalazima kujitetea kama haikujiridhisha kuhusu tuhuma hizo itawaachia huru.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!