Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi ya Zitto Kabwe yaiva
Habari za Siasa

Kesi ya Zitto Kabwe yaiva

Zitto Kabwe akitinga mahakamani Kisutu
Spread the love

UPANDE wa Mashtaka katika mashauri matatu ya uchochezi yanayomkabili Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, umekamilisha upelelezi wa mashauri hayo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi leo tarehe 26 Novemba 2018 mbele ya Hakimu, Huruma Shahidi amedai kwamba upelelezi wa shauri hilo umekamilika.

Baada ya maelezo hayo ya upande wa mashtaka, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imepanga tarehe 13 Desemba mwaka huu kuwa siku ya kumsomea maelezo ya awali (PH), Zitto.

Upande wa utetezi ukiongozwa na wakili Peter Kibatala ulidai kuwa hauna pingamizi juu ya tarehe hiyo.

Zitto anadaiwa kutenda makosa hayo tarehe 28 Oktoba 2018 katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

Habari za Siasa

CCM yakemea ufisadi, yaipa kibarua TAKUKURU

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekemea vitendo vya ubadhirifu wa...

Habari za Siasa

Bajeti ya Ikulu 2024/25 kuongezeka, bunge laombwa kurudhia Sh. 1.1 trilioni

Spread the love  WIZARA ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

error: Content is protected !!