Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi ya Mawio yamponza Mwendesha Mashtaka
Habari za SiasaTangulizi

Kesi ya Mawio yamponza Mwendesha Mashtaka

Spread the love

KWA mara nyingine Mahakama imehoji sababu ya Mwendesha Mashtaka wa Serikali kutoa kauli nyepesi za kushawishi kutoendelea kwa kesi ya tuhuma za uchochezi inayowakabili wahariri wawili. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hakimu Thomas Simba wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu alimtaka Wakili wa Serikali kutilia umuhimu haja ya kuondokana na kauli zinazochelewesha kesi ambayo tayari imechukuwa muda mrefu.

Hakimu Simba anasikiliza kesi Na. 208/2016 inayowakabili mwandishi wa Hali Halisi Publishers Ltd (HHPL), Jabir Idrissa na Mhariri Mtendaji wa MAWIO, Simon Mkina.

Tarehe 30 Aprili, siku ya kutajwa kwa kesi hiyo, upande wa mashtaka kupitia mwanasheria wake alifika mahakamani bila ya jalada la kesi kasoro ambayo Hakimu Simba kaliihoji akisema, “inakuaje tunakuja hapa lakini nyinyi hata jalada la kesi hamnalo?”

Hakimu Simba alisema mtindo huo ni uzembe usiokuwa na sababu na kutaka DPP awe makini kushughulikia kesi anazofungua mahakamani.

Kesi Na: 208 iliyoanza Juni 2016, pia inamkabili mwanasheria na mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (mshtakiwa wa nne) na Ismail Mehboob mshtakiwa wa tatu.

Wakati Mehboob, meneja wa Flint Priting Co, anashtakiwa kwa kosa la kuchapa gazeti lililobeba makala za uchochezi, Lissu anatuhumiwa kutoa maelezo yanayodaiwa kuchochea wananchi waichukie serikali yao.

Lissu alikuwa mmoja wa watu mashuhuri walionukuliwa katika maoni yaliyohusu namna ya kutatua mgogoro wa kisiasa Zanzibar uliozuka baada ya kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi mkuu wa 2015.

Hatua ya kufutwa uchaguzi ilizusha hofu na Lissu katika maoni yake alimtaka Rais John Magufuli kuchukua hatua ya kushughulikia mgogoro huo kabla ya kutokea maafa nchini.

Washitakiwa wote ambao wamekana mashtaka, wako nje kwa dhamana. Kesi itatajwa tena Mei 23.

Kesi ambayo imeanza usikilizaji kwa kutolewa ushahidi na mashahidi wawili, imekuwa ikitajwa tangu Septemba mwaka jana baada ya Lissu kujeruhiwa kwa risasi mjini Dodoma na kulazimika kukimbizwa nje ya nchi kwa matibabu.

Yuko nchini Ubelgiji anakoendelea kutibiwa majeraha yaliyosababishwa na risasi 10 hivi zilizoingia mwilini.

Lissu ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, alishambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 Septemba 7 mwaka jana akiwa anawasili nyumbani kwake Area D Dodoma alikokuwa anashiriki vikao vya Bunge.

Gazeti ambalo lilitumika kufungua mashtaka ya Uchochezi ni MAWIO la Januari 14, 2016 na makala husika kutajwa ni iliyobeba gazeti kwa maneno “Maafa yaja Z’bar.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!