Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Kesi ya kuvunja Muungano yakwama
Habari Mchanganyiko

Kesi ya kuvunja Muungano yakwama

Spread the love

MAHAKAMA ya Afrika Mashariki (EACJ) imetupilia mbali kesi iliyofunguliwa na wananchi ya kupinga Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Uamuzi wa kesi hiyo iliyofunguliwa na Wanzanibar 40,000 wakiongozwa na Rashid Salum Adiy,  umetolewa jana tarehe 19 Septemba 2018 na mahakama ya EACJ.

Hata hivyo, jopo la majaji watano wakiongozwa na Jaji Kiongozi, Monica Mugenyi akiwa na majaji Fakihi Jundu na Dk. Charles Nyawelo waliokuwa wanasikiliza kesi hiyo, waliwashauri walalamikaji kuwasilisha madai yao katika mahakama za Zanzibar.

Katika kesi hiyo, wajibu maombi walikuwa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Katibu Mkuu wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambapo upande huo ulitetewa na Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt. Ally Possi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!