Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi ya Halima Mdee: Hakimu atoa ukomo 
Habari za Siasa

Kesi ya Halima Mdee: Hakimu atoa ukomo 

Halima Mdee, Mbunge wa Kawe
Spread the love

MHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mkuu, jijini Dar es Salaam imetoa ukomo wa kesi inayomkabili Halima Mdee, Mbunge wa Kawe (Chadema) ya kumtolea lugha chafu Rais John Magufuli. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Leo tarehe 26 Agosti 2019, Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba ameutaka upande wa Jamhuri kufunga ushahidi wake kabla ya Oktoba 2019.

Hakimu  Simba ametoa nafasi ya mwisho kwa upande huo kuleta mashahidi waliobakia ili ufunge ushahidi wake na kisha mahakama itoe uamuzi wa kesi hiyo.

Hatua hiyo ya mahakama imekuja baada ya upande wa Jamhuri kushindwa kuleta shahidi katika kesi hiyo.

Upande wa Jamhuri leo ulishindwa kuleta shahidi na kupelekea usikilizwaji wa kesi hiyo kuahirishwa hadi tarehe 4 Septemba 2019.

Wakili upande wa Jamhuri, Sylivia Mitando amedai kwamba wameshindwa kuleta shahidi kutokana na mhusika anaumwa, na kuiomba mahakama hiyo kupanga tarehe nyingine kwa ajili ya kuendelea na ushahidi.

Kesi hiyo ilifunguliwa tarehe 10 Julai 2017, ambapo Mdee anadaiwa kutoka lugha chafu dhidi ya Rais Magufuli akiwa katika Ofisi za Chadema Kinondoni, jijini Dar es Salaam tarehe 3 Julai 2017.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

Habari za Siasa

CCM yakemea ufisadi, yaipa kibarua TAKUKURU

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekemea vitendo vya ubadhirifu wa...

Habari za Siasa

Bajeti ya Ikulu 2024/25 kuongezeka, bunge laombwa kurudhia Sh. 1.1 trilioni

Spread the love  WIZARA ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa...

error: Content is protected !!