Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kenya Airway yapata hasara ya mabilioni
Kimataifa

Kenya Airway yapata hasara ya mabilioni

Ndege ya Shirika la Ndege la Kenya
Spread the love

SHIRIKA la Ndege la Kenya limetangaza kupata hasara ya kiasi cha Shilingi za Kenya 7. 59 Bil (Takriban 151 Bil za Tanzania ) kwa mwaka wa 2018. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Taarifa ya hasara hiyo ilitolewa tarehe 29 Aprili 2019 na jarida maarufu nchini Kenya la masuala ya uchumi na fedha la Business Daily kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Twitter. 

Shirika la Ndege la Kenya limesema, hasara hiyo imetokana na ukubwa wa gharama za uendeshaji ikiwemo kupanda kwa bei ya mafuta na mishahara ya watumishi wa shirika hilo.

Aidha, hasara hiyo ni pungufu ukilinganisha na hasara iliyopata Shirika la Ndege la Kenya kwa mwaka wa fedha wa 2017 ambapo ilikuwa Ksh. 9.44 Bil.

Hata hivyo, shirika hilo limetangaza ongezeko la mapato ya kiasi cha Ksh. 114.45 bilioni ikilinganishwa na mwaka 2017 ambapo yalikuwa ni Ksh. 106.2 bilioni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!