Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kauli ya Prof. Assad baada ya utenguzi
Habari za Siasa

Kauli ya Prof. Assad baada ya utenguzi

Prof. Mussa Assad, aliyekuwa Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali
Spread the love

UTEUZI wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), umefanyika huku, Prof. Mussa Assad akiwa hajui lolote. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Prof. Assad, aliyekuwa CAG kabla ya utenguzi uliofanywa na Rais John Magufuli jana tarehe 3 Novemba 2019, ametoa kauli hiyo wakati akihojiwa na Idhaa ya Kiswahili ya  BBC.

Prof. Assad ameeleza kuwa, alipoteuliwa mwaka 2014 kuwa CAG alipewa barua ya uteuzi, na kwamba alitegemea angepewa barua ya utenguzi wa nafasi hiyo.

“Mimi niliteuliwa mwaka 2014, na nilipoteuliwa barua yangu ilisema kutokana na vifungu kadhaa kadhaa rais ameniteua. Sasa kwa tafsiri yangu nilitaraji barua ya kutokana na vifungu kadhaa rais ametengua uteuzi wangu.

Hilo halijafanyika sababu leo (jana) Jumapili, lakini kesho (leo) Jumatatu barua itakuja. Nitaisoma, tutaona jambo gani nilifanye. Option zote ziko available, hivyo nitajua la kufanya,” amesema Prof. Assad.

Aidha, Prof. Assad amesema kutokana na mazingira yaliyopo, alijua hilo suala ni lazima kutokea.

“Ukitazama mazingira, nilijua hiki kitu ni lazima, lakini nikasema riziki anatoa Mwenyezi Mungu na kwake haiishi. Ikiisha kazi hii ziko kazi chungu mzima za kufanya,” amesema Prof. Assad.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!