Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi nchini (TSNP), Abdul Nondo amesema hawezi kurudi nyuma katika harakati zake za kutetea haki za binadamu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Nondo amesema hayo leo tarehe 5 Novemba 2018, baada ya kuachwa huru na Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa kufuatia kukutwa na hatia katika kesi iliyokuwa ina mkabili ya kujiteka.
Nondo amesema misuko suko aliyopitia imemuongezea nguvu kubwa katika harakati zake na kwamba hawezi rudi nyuma.
Nondo ameachwa huru mara baada ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya mkoa wa Iringa, Liada Chamshana kusema kwamba hana hatia kutokana na upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha madai yao.
Nondo alishitakiwa kwa kesi ya msingi ya kudanganya kuwa alitekwa, na kutoa taarifa za uongo, aliyoyatenda Machi 7, 2018.
Leave a comment