Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ‘Katiba pendekezwa itachochea Wazanzibar kudai uhuru’
Habari za Siasa

‘Katiba pendekezwa itachochea Wazanzibar kudai uhuru’

Othamn Masoud Othman, aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar
Spread the love

OTHMAN Masoud Othman, aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar kabla ya kutimuliwa kwa kuunga mkono mapendekezo ya serikali tatu, amesema Katiba inayopendekezwa  itajenga mfumo utakaosababisha kizazi kijacho cha Zanzibar kidai uhuru badala ya haki ndani ya Muungano, anaandika Pendo Omary.

Othman alifutwa kazi na Dk. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar na nafasi yake kuchukuliwa na Said Hassan Said baada ya kumalizika kwa Bunge Maalum la Katiba 2014, ambapo alipiga kura ya wazi ya kuunga mkono mapendekezo ya serikali tatu kinyume na msimamo wa chama tawala.

Akizungumza katika mkutano wa kwanza wa kitaifa wa Katiba uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Dar es Salaam na kuandaliwa na Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata), Othman amesema;

“Kwa ujumla Katiba inayopendekezwa sio tu kwamba imerasimisha kero za Muungano lakini inajenga mfumo utakaofanya kizazi kijacho cha Zanzibar kidai uhuru badala ya haki ndani ya Muungano.”

Amesema katika kujenga mustakbali wa kikatiba ndani ya Tanzania, suala la Muungano haliwezi kuepukwa kuwa ajenda kubwa na ya msingi.

“Taifa letu limepata uzoefu wa kutosha wa kasoro za Muungano.  Ni dhahiri kuwa itikadi na kutokuwepo upeo na uthabiti katika kujenga mfumo mpya wa kikatiba kumesababisha Katiba inayopendekezwa kuwa mbaya na dhaifu zaidi, katika kujenga mustakbali huo,” amesema Othman.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!