Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kangi: Wanaotumia ajali MV Nyerere kisiasa, watashughulikiwa
Habari za Siasa

Kangi: Wanaotumia ajali MV Nyerere kisiasa, watashughulikiwa

Kangi Lugola Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Spread the love

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewaonya baadhi ya watu wanaotumia ajali ya kivuko cha MV Nyerere kuichonganisha serikali na wananchi wake. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Waziri Lugola ametoa onyo hilo leo alipotembelea Kisiwani Ukerewe kushuhudia shughuli za uokoaji manusura na miili ya watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo.

Waziri Lugola amesema kuwa, watu watakaobainika kuihusisha ajali ya MV Nyerere na tukio la kisiasa wataunganishwa na watu watakao bainika kusababisha ajali hiyo, pindi uchunguzi unaofanywa vyombo vya dola kuhusiana na ajali hiyo utakapokamilika.

“Acheni kutumia tukio hili kisiasa, waache kuchukua tukio hili kama siasa, waache kuchonganisha serikali na wananchi kwa sababu ya tukio hili, hayo ni masuala ya uchochezi, hatuko tayari kupitia tukio hili kugawa watanzania, tukiwabaini tutawakamata, na vyombo vya uchunguzi vitakapokamilika tutawaunganisha nao kwamba wao wanajua zaidi kwa hili lililotokea,” amesema.

Waziri Lugola amewataka waokoaji kuendelea na zoezi la uokoaji manusura na miili ya watu waliopoteza maisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Wagombea 127 wa udiwani kutoka vyama 18 kuchaguliwa kesho

Spread the loveWagombea udiwani 127 kutoka vyama 18 vya siasa wanatarajiwa kupigiwa...

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

error: Content is protected !!