Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kangi: Wanaotumia ajali MV Nyerere kisiasa, watashughulikiwa
Habari za Siasa

Kangi: Wanaotumia ajali MV Nyerere kisiasa, watashughulikiwa

Kangi Lugola Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Spread the love

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewaonya baadhi ya watu wanaotumia ajali ya kivuko cha MV Nyerere kuichonganisha serikali na wananchi wake. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Waziri Lugola ametoa onyo hilo leo alipotembelea Kisiwani Ukerewe kushuhudia shughuli za uokoaji manusura na miili ya watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo.

Waziri Lugola amesema kuwa, watu watakaobainika kuihusisha ajali ya MV Nyerere na tukio la kisiasa wataunganishwa na watu watakao bainika kusababisha ajali hiyo, pindi uchunguzi unaofanywa vyombo vya dola kuhusiana na ajali hiyo utakapokamilika.

“Acheni kutumia tukio hili kisiasa, waache kuchukua tukio hili kama siasa, waache kuchonganisha serikali na wananchi kwa sababu ya tukio hili, hayo ni masuala ya uchochezi, hatuko tayari kupitia tukio hili kugawa watanzania, tukiwabaini tutawakamata, na vyombo vya uchunguzi vitakapokamilika tutawaunganisha nao kwamba wao wanajua zaidi kwa hili lililotokea,” amesema.

Waziri Lugola amewataka waokoaji kuendelea na zoezi la uokoaji manusura na miili ya watu waliopoteza maisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

error: Content is protected !!