Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kangi Lugola azivaa kampuni za ulinzi
Habari za Siasa

Kangi Lugola azivaa kampuni za ulinzi

Kangi Lugola, Waziri wa mambo ya Ndani. Picha ndogo wakati akiapishwa
Spread the love

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, ametoa mwezi mmoja kwa Kampuni binafsi za Ulinzi kuhakikisha yanarekebisha mfumo wao wa kuajiri pamoja na utoaji wa mishahara kabla ya Wizara yake haijaanza kuyahakiki makampuni hayo. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Akizungumza na mamia ya wananchi mjini Bunda, mkoani Mara katika mkutano wa hadhara uliofanyika Stendi ya zamani mjini hapo, Waziri Lugola alisema, Serikali ya awamu ya tano kamwe haitataka uzembe, hivyo makampuni hayo yanayovunja utaratibu huo siku zao zinahesabika.

“La kwanza kabisa makampuni haya yanafanya mambo ya hovyo kwa kuajiri vikongwe kufanya kazi za ulinzi, utamkuta kikongwe kavaa sare ukimuuliza anasema mimi ni mfanyakazi wa kampuni fulani, hii haikubaliki hata kidogo, kwasababu kwa umri ule hawawezi kupambana na wahaarifu, na kwa umri ule muda wote usinzia na baadhi yao unyang’anywa silaha,” amesema Lugola.

Pia lugola amesema kitendo cha baadhi ya makampuni hayo kulipa mishahara midogo, au kutowalipa kabisa wafanyakazi hao, hiyo hali inasababisha uhalifu kwasababu wafanyakazi hao hawataridhika na kipato duni hivyo uweza wakashirikiana na wahalifu au wenyewe kushiriki matukio hayo.

“Nataka makampuni haya yajirekebishe na yasipojirekebisha ndani ya mwezi mmoja ambapo tunataka kuyaakiki makampuni haya, wasije wakamlaumu waziri wa mambo ya ndani ya nchi ambapo yapo baadhi ya makampuni tutaondoa tulichoridhia ili wasifanye kazi katika nchi hii,” amesema Lugola.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!