Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kange Lugola atoa neno kupotea kwa mwandishi wa habari
Habari za Siasa

Kange Lugola atoa neno kupotea kwa mwandishi wa habari

Kange Lugola, Waziri wa Mambo ya Ndani. Picha Azory Gwanda
Spread the love
KANGE Lugola, Waziri wa Mambo ya Ndani, amesema wizara hiyo haihusiki na kupotea kwa mwandishi wa habari wa kampuni ya Mwananchi Communication Limited (Ltd), Azory Gwanda. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Lugola ametoa kauli hiyo, alipoulizwa msimamo wa wizara yake juu ya kupotea mwandishi huyo, Novemba mwaka jana.

Lugola amesema wizara yake haiingilii uhuru wa mtu kwani kitendo cha mtu kuondoka nyumbani kwake na kuelekea pasipojulikana kwani sheria za nchi hazimzuii mtu kutoka sehemu moja na kwenda sehemu nyingine kwani kufanya hivyo si kuvunja sheria.

Waziri Lugola amesema kama Gwanda alitoweka wakati akiwa nyumbani, wao hawahusiki bali wanahusika na mtu aliyetendewa uhalifu ikiwamo kutekwa, akisema katika tukio kama hilo vyombo vya dola humtafuta mtekaji.

“Hawa ambao wanatoweka kwao tu, wanakuwa na sababu nyingi. Kuna wengine maisha yakiwashinda anaamua kwenda kwingine,” amesema.

Lugola alieleza uzoefu wake alipotembelea migodi wakati  akiwa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira). “Kwenye migodi nilikutana na watu ambao kwao walishaweka matanga kwa kujua wameshakufa. Kwao hawaonekani, lakini kumbe wametoweka,” alisema Lugola

Lugola ameeleza kuwa hicho ndicho anachoweza kusema kwa sasa kuhusu kutoweka kwa Gwanda.

Jeshi la Polisi, ambalo jukumu lake kubwa ni kulinda watu na mali zao, liko chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!