Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kamishina wa Magereza afanya mabadiliko
Habari Mchanganyiko

Kamishina wa Magereza afanya mabadiliko

Spread the love

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Tanzania, Phaustine Martin Kasike amefanya mabadiliko ya kiuongozi kwa wakuu wa Magereza wa mikoa na vituo nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa ya mabadiliko hayo imetolewa leo tarehe 24 Julai, 2018 kwa vyombo vya habari na Mrakibu Msaidizi wa Magereza, ambaye pia ni Ofisa Habari Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Lucas Mboje.

Sehemu ya taarifa hiyo inaeleza kuwa, Kamishna Kasike amemhamisha Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dodoma, Naibu Kamishna wa Magereza, DCP Julius Sang’udi kwenda Makao Makuu ya Magereza kuwa Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Wafungwa. huku nafasi yake ikichukuliwa na Mkuu wa Magereza wa Singida, Kamisha Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, SACP Salum Hussein.

Nafasi ya SACP Hussein imechukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Magereza, ACP Msepwa Omary aliyekuwa Mkuu wa Gereza la Mtego wa Simba. ACP Msepwa amekuwa Kaimu Mkuu wa Magereza mkoa wa Singida na nafasi yake kukaimiwa na Mrakibu wa Magereza, Muta Tibalinda.

Vile vile, taarifa hiyo inaeleza kuwa, Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga Naibu Kamishna wa Magereza, DCP John Masunga amehamishiwa Makao Makuu ya Magereza kuwa Mkuu wa Kitengo cha Viwanda vya Jeshi la Magereza ambapo nafasi yake imekaimishwa kwa aliyekuwa Mnadhimu wa Magereza Mkoani Tanga, Kamishna Msaidizi wa Magereza, ACP Emmanuel Lwinga.

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!