Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kamanda Shana afariki dunia
Habari Mchanganyiko

Kamanda Shana afariki dunia

Jonathan Shana (katikati) aliyekuwa Ofisa Mnadhimu wa Chuo cha Polisi Moshi (CCP),
Spread the love

ALIYEKUWA Ofisa Mnadhimu wa Chuo cha Polisi Moshi (CCP), Jonathan Shana amefariki dunia Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Shana aliyewahi kuwa Kamanda wa Polisi mikoa mbalimbali ikiwemo Simiyu, Pwani, Mwanza na Arusha amefikwa na mauti usiku wa kuamkia leo Jumatano tarehe 16 Septemba 2020.

Msemaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Aminiel Aligaesha amethibitisha kutokea kwa kufo hicho cha Kamanda Shana akisema amefikwa na mauti baada ya kualazwa hospitalini hapo kwa siku 21 kati ya hizo tatu alikuwa chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi (ICU).

Enzi za uhai wake, Kamanda Shana alikuwa akionekana kujihusisha na shughuli za vyama vya siasa akiwa amevalia sare za polisi jambo ambalo lilikuwa likiibua mjadala.

 

Mrisho Gambo, aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Arusha wakati Shana akiwa kamanda wa polisi wa mkoa huo, ameandika katika ukurasa wake wa Instagram “nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Kamanda Shana.”

“Wiki iliyopita nilikwenda kumuona Muhimbili ambako alilazwa karibuni wiki tatu na nilipata matumaini makubwa. Jaman Kamanda Shana! Bwana ametoa na ametwaa – Jina la Bwana libarikiwe,” ameandika Gambo ambaye kwa sasa ni mgombea ubunge Arusha Mjini kupitia CCM

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!