Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kali ya mwaka: JPM atumbua, ateua hapo hapo
Habari za SiasaTangulizi

Kali ya mwaka: JPM atumbua, ateua hapo hapo

Aliyekuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Kisarawe (DAS ), Mtela Mwampamba
Spread the love

RAIS John Magufuli amemtumbua hadharani Katibu Tawala wa Wilaya ya Kisarawe (DAS ), Mtela Mwampamba na kumteua Mwanana Msumi kushika nafasi hiyo hapo hapo. Anaripoti Hamisi Mguta…(endelea).

Mwambapa ametumbuliwa leo tarehe 28 Juni 2020, wakati Rais Magufuli akizindua mradi wa maji wilayani humo katika Mkoa wa Pwani.

“….lakini pia hapa kuna tatizo moja, la mteule wangu mmoja DAS, nimeambiwa ana mambo ambayo hayaendani na maadili ya kazi yake, kwamba anachukua hata wake za watu. nilikwishamuonya siku za nyuma, nafikiri hakuweza kuonyeka.

“Na kwa sababu jukumu langu ni pamoja na kusimamia maadili nanidhamu za watendaji, ninakuagiza muheshimiwa Jafo (Suleiman Jafo – Waziri wa TAMISEMI) uongee na mheshimiwa Mkuchika (George Mkuchika, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora) kwamba huyu kazi ya U-DAS nimeitengua leo,” amesema Rais Magufuli.

Pia Rais Magufuli ameagiza Mwampamba atafutiwe kazi ya chini inayoendana na uwezo wake, lakini pia kazi hiyo asifanye ndani ya Wilaya ya Kisarawe. Aliuliza kama ndani ya wilaya hiyo yupo anayefaa, na yafuatayo ndio mazungumzo yalivyokuwa:-

Rais John Magufuli

Rais Magufuli: Kwa hiyo utamueleza Mkuchika aniletee mapendekezo, au kama yupo hapa mnayemuona mwingine anayefaa faa U-DAS nimpe, kisha akamwita Mkuu wa Mkoa.

Rais Magufuli: Mkuu wa Mkoa… (Mhandisi Evarist Ndikilo).

Mkuu wa Mkoa: Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe kuna Afisa Tawala, anaweza kabisa kufanya kazi hiyo.

Rais Magufuli: Ofisa Tawala yupo hapa? Njoo hapa ofisa tawala

Rais Magufuli: Ana elimu gani?

Aliyekuwa Afisa Tawala wilaya ya Kisarawe, Mwanana Msumi

Ofisa Tawala: Masters in Public Administration

Rais Magufuli: Una Masters ya Public Administration. Kuanzia leo wewe ni DAS, uendelee kufanya kazi, ili na nyinyi sana mkagombanie wanaume na Mkuu wa Wilaya (Jokate Mwegelo), halafu wote muondoke, ila hongera mama.

Rais Magufuli: Haya muandikieni barua leo aipate, huyu ndio DAS wa Kisarawe, sawa jamani? Mwanana Msumi oyeeee!

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

error: Content is protected !!