Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Kakolanya aishika pabaya Yanga
Michezo

Kakolanya aishika pabaya Yanga

Makao Makuu ya Klabu ya Yanga
Spread the love

UONGOZI wa klabu ya Yanga umekili kupokea barua kutoka kwa mwanasheria wa mlinda mlango wao Benno Kakolanya kutaka kuvunja mkataba na timu hiyo licha ya kulipwa stahiki zake zote alizokuwa akidai hapo awali. Anaripoti Kelvin mwaipungu… (endelea)

Kaimu M/nyekiti wa klabu hiyo Samuel Lukumay alikili uongozi wa klabu hiyo kupokea barua ya pili kutoka kwa mchezaji huyo 28 january, 2019 ambayo alikuwa akisisitiza kutaka kuvunja mkataba na timu hiyo licha ya kulipwa stahiki zake zote.

“Benno aliuandikia uongozi barua ya siku 14 ambayo ilikuwa ni ‘notice’ kumlipa haki zake au kuvunja mkataba kama uongozi ilibidi kufanya juhudi ili kumlipa stahiki zake kama ambavyo tunawalipa wachezaji wenzake na Benno akawa amelipwa madai yake yote na tumewajibu wanasheria wake kwa barua kuwa kile alichokuwa anadai tumeshamlipa”

“Tulichokipata tena kutoka kwa wanasheria wake ni barua ya msisitizo wa kutaka kuvunja mkataba ambayo tumeipata siku ya jana” alisema Lukumay

Ikumbukwe Benno ameingia kwenye mgogoro na klabu hiyo baada ya kutaka kulipwa mshahara wake wa miezi mitatu pamoja na fedha ya usajiri ambayo hakumaliziwa kiasi cha kususa kuingia kambini wakati timu hiyo ikijiandaa na mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Mwadui Fc.

Baada ya mchezaji huyo kutoripoti kambini kocha mkuu wa klabu hiyo Mwinyi Zahera alisema kuwa hamhitaji tena mchezaji huyo ndani ya kikosi chake licha ya kulipwa stahiki zake zote kwa kuwa anaweza kuleta mpasuko ndani ya timu kwa kuwa wachezaji wanaodai ni wengi.

Kwa sasa klabu ya Yanga ina hali ngumu ya kifedha toka alipojihudhulu  aliyekuwa M/nyekiti wa klabu hiyo Yusuph Manji ambae pia alikuwa kama mfadhili mkuu.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

error: Content is protected !!