Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kabendera kupandishwa kizimbani
Habari Mchanganyiko

Kabendera kupandishwa kizimbani

Erick Kabendera
Spread the love

MWANDISHI wa Habari, Erick Kabendera kesho tarehe 1 Agosti 2019 anatarajiwa kupandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kabendera anayetuhumiwa kuwa sio raia wa Tanzania, atapandishwa kizimbani hapo kesho majira ya saa tatu asubuhi. Baada ya Mtandao wa Kutetea Haki za Binadamu (THRDC) kupitia mawakili wake, kufungua maombi ya dhamana Namba 14 ya mwaka 2019.

Kabendera anatetewa na Mawakili Jones Sendodo, Shilinde Swedy na Catherine Ringo kutoka mtandao wa THRDC.

Loy Kabendera mke wa Kabendera leo tarehe 31 Julai 2019 ameruhusiwa kumuona mume wake ikiwa zimepita siku mbili tangu alipokamatwa na jeshi la Polisi tarehe 29 Julai mwaka huu, akiwa nyumbani kwake Mbweni Jijini Dar es salaaam.

Kwa mujibu wa THRDC, Kanbendera anashikiliwa katika Kituo cha Polisi cha Kilwa Road.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

error: Content is protected !!