Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kabendera aanza kuona nuru
Habari Mchanganyiko

Kabendera aanza kuona nuru

Mwandishi Erick Kabendera akiwa mahakamani
Spread the love

MAZUNGUMZO ya kukiri makosa kati ya mwandishi wa habari za uchunguzi, Erick Kabendera na Mkurugenzi wa Mashtaka Tanzania (DPP) yapo kwenye hatua ya mwisho. Anaripoti Martin Kamote, Dar es Salaam … (endelea).

Hayo yameelezwa leo tarehe 11 Februari 2020, kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na Faraja Nchimbi, Wakili wa Serikali Mkuu, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Janeth Mtega.

Wakili Nchimbi ameieleza mahakama hiyo, kuwa upande wa mashtaka na ule wa utetezi upo kwenye majadiliano ya kukiri kwa muda mrefu sasa na yanafikia mwishoni.

Wakili Nchimbi ameiomba Mahakama kufanya mazungumzo binafsi na mshtakiwa Kabendera ili mtuhumiwa akubali kukiri mashtaka yake na kuendelea na taratibu nyingine za kisheria.

Nchimbi ameiomba mahakama hiyo kuhairisha shauri hilo mpaka tarehe 17 Februari mwaka huu.

Wakili wa Utetezi, Jebra Kambole ameieleza mahakama hiyo kuwa upande huu haupingi jamhuri kuzungumza na mtuhumiwa huyu.

Hakimu Mtega ameruhusu mazungumzo hayo na kuahirisha shauri hilo mpaka tarehe 17 Februari 2020.

Mazungumzo hayo yapo kisheria kifungu cha 3 na kuongeza kifungu cha 194 A 194 H cha sheria ya Makosa ya jinani ya mwaka 1985 sura ya 20 (Plea Bargaining), ambapo mtuhumiwa anapewa nafasi ya kukiri na kuiomba msamaha na baadaye kuachiwa huru.

Hivyo huenda Kabendera huenda Jumatatu akaachiwa huru kutokana na mazungumzo hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!