Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM: Mtalii hatowekwa karantini
Habari za Siasa

JPM: Mtalii hatowekwa karantini

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli amemwagiza Dk. Hamisi Kigwangalla, Waziri wa Utalii na Injinia Isack Kimwelwe, Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano kuruhusu ndege za utalii kutoka nje, na kwamba mtalii hatowekwa karantini. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam…(endelea).

Msimamo huo ameutoa leo tarehe 17 Mei 2020, katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Ushirika wa Chato, alipokwenda kufanya ibada.

“Mpaka ninapozungumza hapa, kuna masharika ya ndege ambayo siwezi kuyataja yashabook (orodhesha) watalii wengine mpaka mwezi wa nane, ndege zimejaa kwa ajili ya kuja Tanzania kuanza kutalii, wanakuja kwa sababu wanaujua ukweli wanakuja kwa sababu Tanzania ni pazuri,” amesema.

Amesema, watalii hao wakifika nchini, hawatawekwa karantini isipokuwa watapimwa joto lao la mwili kisha kuruhusiwa.

“…nimeishatoa maagizo kwa Waziri wa Maliasili na Waziri wa Uchukuzi waruhusu hizo ndege ziingie, na wala hawatawaweka karantini. Wakishafika hapa, akishapimwa akakutwa na temperature (joto) ipo kawaida, hana dalili za corona aendee akaangalie wanyama huko…,”amesema na kuongeza:

“Hatuwezi sisi kama taifa huru tukakubali corona itawale, Mungu wetu atatawala lakini corona haitatawala.… Tukiufanya uchumi wetu ukalala, hata mishahara hatutalipa.”

Rais Magufuli amewataka Watanzania kuondoa na hofu, kwa kuwa hofu ni ugonjwa mbaya kuliko corona “nitoe wito kwa Watanzania, kuna maneno mengi yaliyotiwa chumvi, hofu ni ugonjwa mkubwa kuliko corona.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!