Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM azungumzia uchaguzi 2020, aonya wanaopanga kufanya fujo
Habari za Siasa

JPM azungumzia uchaguzi 2020, aonya wanaopanga kufanya fujo

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli amewataka Watanzania kujiandaa vyema, katika kushiriki Uchaguzi Mkuu  wa mwaka huu.Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Rais Magufuli ametoa wito huo wakati akitoa salamu za kheri ya mwaka mpya kwa Watanzania, leo tarehe 11 Januari 2020, katika ziara yake Visiwani Zanzibar .

“Mwaka huu uwe wa amani na mafanikio, kama mjuavyo baadae mwaka huu nchi yetu inafanya uchaguzi mkuu, hivyo nawasihi wote tujiandae kushiriki uchaguzi huo vizuri. Na bila kusahau kumuomba Mungu aendelee kulilinda na kulisimamia taifa letu,” amesema Rais Magufuli.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amewaonya watu wanaopanga kufanya fujo katika uchaguzi huo.

“Ukiona kuna amani ujue kuna watu hawalali, kwa sababu wale ambao wangependa nchi hii isiwe na amani wapo, na vibaraka hawaishi walikuwepo hata enzi za mitume. Hata Mungu aliumba malaika lakini wengine waligoma wakata wawe kama yeye akawafukuza wakawa mashetani.

Kwa hiyo vibaraka wataendelea kuwepo, saa nyingine mnaweza kufanya uchaguzi ukamaliza mwingine akasema nitaapishwa tu, msubiri nitakuja kuapishwa,” ameeleza Rais Magufuli

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!