RAIS John Magufuli amewataka Watanzania kujiandaa vyema, katika kushiriki Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).
Rais Magufuli ametoa wito huo wakati akitoa salamu za kheri ya mwaka mpya kwa Watanzania, leo tarehe 11 Januari 2020, katika ziara yake Visiwani Zanzibar .
“Mwaka huu uwe wa amani na mafanikio, kama mjuavyo baadae mwaka huu nchi yetu inafanya uchaguzi mkuu, hivyo nawasihi wote tujiandae kushiriki uchaguzi huo vizuri. Na bila kusahau kumuomba Mungu aendelee kulilinda na kulisimamia taifa letu,” amesema Rais Magufuli.
Wakati huo huo, Rais Magufuli amewaonya watu wanaopanga kufanya fujo katika uchaguzi huo.
“Ukiona kuna amani ujue kuna watu hawalali, kwa sababu wale ambao wangependa nchi hii isiwe na amani wapo, na vibaraka hawaishi walikuwepo hata enzi za mitume. Hata Mungu aliumba malaika lakini wengine waligoma wakata wawe kama yeye akawafukuza wakawa mashetani.
Kwa hiyo vibaraka wataendelea kuwepo, saa nyingine mnaweza kufanya uchaguzi ukamaliza mwingine akasema nitaapishwa tu, msubiri nitakuja kuapishwa,” ameeleza Rais Magufuli
Leave a comment