Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM awaweka njia panda Dk. Kigangwalla, Prof. Mkenda
Habari za Siasa

JPM awaweka njia panda Dk. Kigangwalla, Prof. Mkenda

Spread the love

RAIS John Magufuli ametoa siku tano kwa Dk. Hamisi Kigwangalla, Waziri wa Maliasili na Utalii na Prof. Adolf Mkenda, Katibu Mkuu wa wizara hiyo, kuondoa tofauti zao vingenevyo ‘atawatumbua’. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo tarehe 31 Desemba 2019, wakati akizungumza na Maafisa na Askari wa Wanyamapori wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo ….

Kiongozi huyo wa nchi amesema mahusiano mabaya ya  Dk. Kigwangalla na Prof. Mkenda yanasababisha baadhi ya shughuli za wizara hiyo, kukwama.

“Nnafahamu watendaji wenu wa juu Katibu Mkuu wa Wizara kila siku wanagombana, na ninawatazama taratibu. Nilishampa kazi Katibu Mkuu Kiongzi awaite, awaeleze lakini wasipobadilika nitawaondoa. Hilo ni lazima nizungumze kwa dhati,” ameagiza Rais Magufuli na kuongeza;

“Siwezi kuwa na watendaji wa kuteua mimi halafu kila siku wanagombana, kuna mambo mengi hayaendi. Katibu Mkuu hamheshimu Waziri n Waziri nae hataki kwenda na Katibu Mkuu, siwezi kuvumilia hilo.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!