Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa JPM ateta na Rais Nyusi kwa simu
Kimataifa

JPM ateta na Rais Nyusi kwa simu

Rais wa Msumbuji, Filipe Nyusi (kushoto) akiwa na mwenyeji wake Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli amefanya mazungumzo kwa simu na Rais wa Msumbuji, Filipe Nyusi kuhusu masuala mbalimbali yahusuyo uhusiano na ushirikiano baina ya mataifa hayo mawili ya Bara la Afrika. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa iliyotolewa leo Jumatano tarehe 1 Julai 2020 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa amesema, Rais Magufuli amempongeza na kumtakia heri Rais Nyusi na wananchi wote wa Msumbiji kwa Taifa hilo kuadhimisha miaka 45 ya tangu kupata uhuru wake.

Rais Magufuli amemueleza Rais Nyusi kuwa Tanzania itaendeleza ushirikiano na uhusiano mzuri wa kidugu, kirafiki na ujirani mwema na Msumbiji kama ulivyoasisiwa na Baba wa Taifa la Tanzania, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Hayati Samora Mosës Machel wa Msumbiji katika masuala mbalimbali yakiwemo ya kiuchumi na kijamii.

Aidha, viongozi hao wamezungumzia maandalizi ya kupokezana kijiti cha uenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ambapo Rais Magufuli ambaye ni Mwenyekiti wa sasa wa SADC atamkabidhi uenyekiti wa SADC, Rais Nyusi ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa SADC kwa sasa.

Viongozi hao pia wamezungumzia ugonjwa wa homa ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona (COVID-19) ambapo wamebadilishana mawazo juu ya namna bora ya kukabiliana na ugonjwa huo, hasa namna Tanzania ilivyofanikiwa kupunguza maambukizi yake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!