Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM: ATCL imekusanya Bil. 32.7
Habari za Siasa

JPM: ATCL imekusanya Bil. 32.7

Spread the love

RAIS John Magufuli amesema Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) limekusanya mapato, kiasi cha Dola 14 milioni (sawa na TSh. 32.7 bilioni). Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Rais Magufuli amesema hayo leo tarehe 26 Oktoba 2019, katika hafla ya upokeaji ndege mpya ya serikali aina ya Boeing 787-8 Dreamliner, iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Rais Magufuli amesema mapato hayo yametajwa na Mhandisi Isack Kamwelwe, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, na kuwa,  atafuatilia mapato hayo kama ni kweli.

“Hizi zimenunuliwa kwa fedha za serikali hazijanunuliwa na ATCL, tumewaazima wazitumie kufanya biashara, na biashara lazima izalishe. Nilimuuliza waziri amesema wana Dola 14 miliono, nitakwenda kuzicheki kesho kwenye akaunti,” amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli ameuagiza uongozi wa ATCL kutekeleza majukumu yao vizuri, ili shirika hilo lijiendeshe kwa faida.

“Nitoe wito, kwanza kwa management (uongozi) na watumishi wa ATCL, tekelezeni majukumu yenu vizuri,” amesema Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!