Friday , 29 March 2024
Habari za Siasa

JPM amtumbua mwingine

Rais John Magufuli
Spread the love

WAKILI Julius Kalolo, ameteuliwa na Rais John Magufuli kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Wakala wa Umeme Vijijini (REA). Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Taarifa ya uteuzi huo imetolewa jana tarehe 17 Juni 2019 na Mkurugenzi wa Mawasiliani ya Rais-Ikulu, Gerson Msigwa.

Taarifa ya Msigwa inaeleza kuwa, uteuzi wa Wakili Kalolo umeanza rasmi jana.

Aidha, taarifa hiyo imeeleza kwamba uteuzi wa Wakili Kalolo umefuatia hatua ya Rais Magufuli kutengua uteuzi wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya REA, Michael Nyagoga.

“Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Bw. Michael Pius Nyagoga kuanzia leo (jana) tarehe 17 Juni, 2019,” imeeleza taarifa ya Msigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!