Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM amnanga RC aliyemtumbua
Habari za Siasa

JPM amnanga RC aliyemtumbua

Spread the love

RAIS John Magufuli amemnanga Dk. Steven Kebwe, aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kwa madai ya ‘kujimegea.’ Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Amesema, alijisahau na baadhi ya miradi kwenye halmashauri ilikuwa yake, akieleza mfano kwamba alipeleka mbao za hoyo kwenye halmashauri moja mkoani humo.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo tarehe 20 Novemba 2019, mkoani Morogoro wakati akizungumza na wakazi wa mkoa huo.

Amemsifu mkuu wa mkoa huo wa sasa, ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Arusha, Loota Sanare kwamba ameanza kazi vizuri.

“…umeanza vizuri, endelea kuchaa kazi. Umeanza vizuri endelea kushughuikia kero zote, nataka niseme wazi, mkuu wa mkoa aliyekuwepo alijisahau.

“Baadhi ya miradi mingine hata kwenye halmashauri ilikuwa yake, kuna halmashauri ali – supply mbao za ovyo, ninayajua yote,” amesema Rais Magufuli.

Akimsife Sanare, Rais Magufuli amesema, ameanza kushughulikia kero za wananchi wa Morogoro na kumwagiza kuendelea kukabili matatizo ya mkoa huo.

“Shughulikia kero za wananchi hawa, shughulikia migogoro ya wafugaji na wakulima, nayo iishe sababu saa nyingine wakati wa kilimo, wakulima wanalima huku wafugaji wanakwenda kulisha mazao.

“Wanapeleka ng’ombe kwenye mazao, nimekuleta uwadhibiti hapa, ili Morogoro iwe na amani, wananchi waishi kwa amani,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!