Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Josephat Isango afariki dunia asubuhi hii
Habari MchanganyikoTangulizi

Josephat Isango afariki dunia asubuhi hii

Spread the love

MWANDISHI wa habari Josephat Isango amefariki dunia mapema asububi leo, anaandika Hamisi Mguta.

Taarifa za kifo chake zimethibitishwa na mdogo wake aitwae Christopher ambaye amekuwa akimuuguza.

Christopher amezungumza na Mhariri wa gazeti la MwanaHALISI Jabir Idrissa na kusema Isango amefia hospitalini Ikungi mkoani Singida.

Isango alilazwa hospitalini hapo kwa wiki mbili sasa akisumbuliwa na kifua. Hata hivyo uchunguzi wa afya yake ulibaini ana tatizo kwenye moyo.

Aliwahi kuugua akiwa jijini Dar es Salaam na baada ya muda mfupi aliamua kusafiri kwenda Singida, mkoa wa nyumbani kwao.

Isango amekuwa mwandishi wa habari maarufu kutokana kuhusika na matukio ya kuvutana na polisi.

Josephat Isango enzi za uhai wake aliposhambuliwa na polisi

Mwaka 2015 alishambuliwa na polisi wa FFU eneo la mbele ya makao makuu ya Jeshi la Polisi katikati ya jijini Dar es Salaam alipokuwa na waandishi wengine wakisubiri kuwasili kwa viongozi wakuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Viongozi wa Chadema waliitwa na Jeshi hilo kwa ajili ya mahojiano kuhusiana na tuhuma za kuchafua amani.
Kwa karibu miaka miwili, Isango alifanyakazi kampuni ya Hali Halisi Publishers Ltd (HHPL) inayomiliki na kuchapisha gazeti la MwanaHALISI na kuendesha mitandao ya kijamii.

Josephat Isango enzi za uhai wake akiwa katika majukumu yake ya kazi

Alihamia akitoka kampuni ya Free Media inayomiliki na kuchapisha gazeti la Tanzania Daima. Lakini alipata kuandika habari na makala MwanaHALISI kwa njia ya kujitegemea tangu mwaka 2008.

Isango, mzaliwa wa kijiji cha Kisasida, mkoani Singida, alisomea uandishi wa habari Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine Nyegezi jijini Mwanza.
Alikuwa mmoja wa waandishi wenye ujasiri wa kukabiliana na mazingira magumu ya kazi.

Alipoamua kuhama MwanaHALISI mhariri wake alisema itamchukua muda mrefu kupata mwandishi kijana mkakamavu kama Isango.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

error: Content is protected !!