Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu JK awakaribisha wanafunzi UDSM, autega uongozi Dar
Elimu

JK awakaribisha wanafunzi UDSM, autega uongozi Dar

Spread the love

JAKAYA Kikwete, Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) nchini Tanzania, amewakaribisha wanafunzi wa chuo hicho kuendelea na masomo. Anaripoti Mwandishi wetu, Dar es Salaam … (endelea)

Kikwete ambaye pia ni Rais mstaafu wa Tanzania, amesema hayo leo Alhamsi tarehe 28 Mei, 2020 mara baada ya kutembelea Hosteli za Magufuli jijini Dar es Salaam zinazotumiwa na wanafunzi wa UDSM.

Hosteli hizo zilikuwa zikitumika kama karantini kwa watu kukaa hapo kwa siku 14 ili kuangalia kama wana maambukizo ya ugonjwa unaosababishwa na virusi vya corona (COVID-19).

Matumizi hayo ya hosteli yalifanyika baada ya vyuo kuwa vimefungwa kuanzia tarehe 18 Machi, 2020 kutokana na kuwepo kwa ugonjwa wa corona nchini. Vyuo vyote vitafunguliwa tarehe 1 Juni, 2020.

Katika ziara yake leo, Rais mstaafu Kikwete kabla ya kuwakaribisha wanafunzi, amepokea maelezo kutoka kwa Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Dar es Salaam, Neema Kwemba ambaye alimhakikishia ziko salama.

 

Neema amesema, zaidi ya mwezi sasa hosteli hizo zilikuwa hazitumiki na walifanyan utakasaji wa majengo yote, vyubani, magodoro na kila eneo lote.

Baada ya maekezo hayo, Kikwete akasema, “tunaichukua kauli yenu kwamba pako salama, nataka kuwahakikishia tena vijana, pako salama njooni, kwani tuliowakabidhi wamefanya kama tulivyokubaliana.”

Huku akifurahi, Kikwete akasema, “Basi likitokea la kutokea tutawasiliana, tujue, je wamekuja nao ama wameupatia hapa. Kwa niaba ya chuo kikuu tunawashukuru.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

error: Content is protected !!